PEPTIC ULCERS
almaarufu kama Vidonda Vya Tumbo
hutokea hasa pale ambapo mtu hana kitu kinachoepusha acid iliyomo ndani ya
tumbo kutafuna kuta za tumbo lake. Ulcers
hutokea si kwenye tumbo tu, bali pia na katika mwanzo wa utumbo mdogo (Duodenum) na hivyo kuitwa Duodenal Ulcers.
JINSI ULCERS INAVYOTOKEA
JINSI ULCERS INAVYOTOKEA
Ndani ya
tumbo lako, kuna substances
vinavyopatikana ndani ya tumbo navyo hujulikana kwa majina Hydrochloric Acid (HCl) na Pepsin
Enzyme. Hizi mbili hutumika katika kumeng’enya chakula kilichomo
tumboni lakini ukosefu wa chakula ndani ya tumbo lako hupelekea substances hizi kujijenga kwa haraka na
kuanza kuharibu mistari iliyoko ndani ya tumbo ama Gastrointestinal-GI Tract.
Ulapo chakula
acid hiyo ambayo huwa katika ukali unaoendana na hali ya tumbo lako husafishwa
na chakula hicho lakini kwa wakati mfupi na ikitumika kama kivunjio cha
virutubisho vinavyopatikana kwenye chakula.
Acid hii hurudi
mara kwa mara ili kuendelea kutafuta chakula cha kumeng’enya kupata virutubisho
vihitajiwavyo na mwili na chakula hicho kinapokosekana ndipo pale ambapo acid
inamwagika katika kuta za tumbo na hivyo kupelekea vidonda kutokea. Hali ya
vidonda hivi kuwemo ndani ya tumbo na urudiaji wa kumwagika kwa acid hii
huchokoza vidonda hivi na hivyo kuvitonesha na kukupelekea kusikia uvimbeuchungu
au moto ndani ya tumbo au zaidi maumivu makali.
Utafiti
umesema kuwa zaidi ya wagonjwa 35% wenye ulcers hupatwa na matatizo mengine
ambayo mengi huweza kuzuilika. Wachache hupatwa na Perforation of the Lining GI
(Gastrointestinal) Tract (kitobo
katika kuta za mistari ya tumbo) na kuvuja kwa damu ndani kwa ndani.
VISABABISHI VIKUU
VISABABISHI VIKUU
Vidonda vya
Tumbo husababishwa mara kwa mara na mambo tofauti ambayo hatuna budi sisi
wanadamu kuwa nayo. Uchunguzi uliofanywa miaka ya 1980 nchini Marekani
ulisimamia kwamba Ulcers za aina yeyote ile husababishwa sana na mtu kuwa na
stress ya kupindukia.
Lakini uchunguzi huu ulikanushwa miaka hii ya hivi karibuni na Madaktari huku wakisema kwamba Ulcers husababishwa na mambo yafuatayo;
Lakini uchunguzi huu ulikanushwa miaka hii ya hivi karibuni na Madaktari huku wakisema kwamba Ulcers husababishwa na mambo yafuatayo;
1.Msongo mkubwa wa Mawazo
2.Utumiaji wa madawa ya kulevya aina ya Anti Inflamatory Drugs(NSAIDs kama Aspirin)
2.Utumiaji wa madawa ya kulevya aina ya Anti Inflamatory Drugs(NSAIDs kama Aspirin)
3.Mfumo mbovu wa Maisha (Poor Lifestyle)
4.Maambukizi ya Bacteria. Maambukizi
haya husababishwa na bacteria Helicobacter
pylori - H. pylori wanaosambazwa na maji
DALILI ZA ULCERS
DALILI ZA ULCERS
Hatuwezi
kukimbilia kuelezana jinsi ya kuua ulcers ulizonazo bila ya kuelezena dalili
zake. Kwa wengi ulcers haziumizi tu bali pia huweza kuleta matatizo kama maradhi, kubadilika kwa ladha mdomoni, kutapika n.k. Unataka kujua jinsi
ulcers zianzavyo, zifuatazo ni dalili kuu zinazosababishwa na ulcers;
1.
Maumivu sehemu ya kiuno (baada
ya kula) na Kichomi (sehemu kati ya tumbo na kifua)
2.
Kutapika damu au kukojoa damu au
kinyesi chenye damu
3.
Nausea na Kutapika
4.
Kinyesi kuwa cheusi
5.
Kukosa hamu ya kula na kupungu
uzito
6.
Kukosa usingizi kwa sababu ya
maumivu makali usiku
7.
Tumbo kujaa gesi
8.
Upungufu wa maji mwilini na
kuishiwa na nguvu.
JINSI YA KUPUNGUZA NA KUUA VIDONDA VYA TUMBO
JINSI YA KUPUNGUZA NA KUUA VIDONDA VYA TUMBO
Nadhani hadi
tulipofikia, inafaa sasa kuelezana jinsi ya kuua vidonda vya tumbo. Njia zote
ni rahisi hasa kama utazingatia mwenendo wa lifestyle yako wewe mwenyewe:
1.
Punguza
kuwa na msongo wa mawazo (reduce overstressing).
Siku
moja imetokea kwamba umepatwa na tatizo moja la kuondokewa na kitu au mtu
umpendaye kwa dhati, ni kawaida kwetu sisi wanadamu kuwakumbuka tuliopotelewa
nao lakini ni hali ya kila mwanadamu kupotelewa na kitu aghalabu mtu maishani
mwake. Jambo hili lisiwe gheni kwako kwa kuwa utakuwa ndani ya mateso yako wewe
mwenyewe.
Unapokuwa
na msongo wa mawazo ni dhahiri kwamba unatoa nafasi kwa ulcers kuingia katika
maisha yako. Upotewapo na mtu, huna budi kuwa katika hali ya mawazo, kufukuzwa
kazi pia utakuwa katika hali hiyo hiyo au mpenzi wako unayempenda kupitiliza
akakutema ndiyo hapo utakapotamani dunia ipasuke na kukumeza. Yaache yaliyopita
yawe yamepita.
Uchunguzi
umesema kuwa msongo wa mawazo humfanya mgonjwa wa ulcers kuyakaribisha maumivu
makali ndani ya maisha yake kwa kuwa mfumo wa kumeng’enya chakula (Digestive system) unauhusiano wa moja
kwa moja na ufanyakazi wa ubongo (Gut-Brain
Connection).
Mwili
hutuma signals za uwoga, hofu, huzuni,
msongo wa mawazo, kukosa raha na hata depression (sonona) kwenda kwenye
ubongo hivyo kuyapa magonjwa tajwa mwanzo nafasi.
IIi
kuweza kuendesha mawazo yako, tazama Jinsi ya kuzuia msongo wa mawazo au tumia dawa
asilia za kuzuia msongo wa mawazo kama kufanya mazoezi mara kwa mara,
meditating, kusali, kutembea kila jioni sehemu mbalimbali jijini kwako, kupata
usiingizi wa kutosha n.k.
2.
Punguza
matumizi ya Dawa za kutuliza maumivu (NSAID Pain Relievers)

Watu wengi huzitumia mara kwa mara bila ya kujua kwamba zinamadhara wakitegemea kwamba zitawasaidia moja kwa moja.
Kiujumla
dawa hizi husababisha magonjwa mengine yawe sugu ndani ya mwili wa mtu kwa
sababu magonjwa hayo yatakuwa na tabia ya kujirudia mara kwa mara. Maumivu huwa
makali hasa pale ambapo gonjwa limejirudia kwa mara ya tatu kama Kuumwa na kichwa (headache), maumivu ya viungo
vya mwili (joints of the body), misuli kukaza (muscle cramps), misuli
kuchanika (muscle tearing), homa (fever), na kadhalika.
Ushauri
umetolewa kwamba mgonjwa mwenye vidonda vya tumbo asitegemee sana dawa za
kupunguza maumivu kwani ufanyaji kazi wa akili huwa na uhusiano wa moja kwa
moja na tumbo. Utafiti umesema kwamba mtu huyu atajisababishia vidonda kwenye
kuta za tumbo na hivyo kujiweka hatarini na maumivu makali zaidi.
Ninukuu
kutokusema kwamba usizitumie dawa hizi bali ninukuu kusema kwamba usizitegemee
sana. Kupunguza kutumia dawa hizi husaidia kuepusha utengenezaji wa acidi
inayochoma vidonda ndani ya tumbo. Zitumie dawa hizi kulingana na ushauri wa
daktari kwa muda aliokushauri uzitumie. Usizidishe hata kama umeona hujapona,
utajizidishia maradhi.
3.
Tafuta
tiba mbadala
Nenda
hospitali ukapate matibabu kamilifu yanayoweza kukupa njia ya kuepukana na
uvimbeuchungu (Inflammations) zinazosababishwa na H. pylori ambaye huumiza
tumbo na utumbo mdogo kwa kuutafuna na kutengeneza mikato ambayo ni migumu
kupona. Huweza kusababisha pia kuvuja damu kwa ndani.
Helicobacter pylori
huharibu kamasi (mucous coating) linalopatikana kwenye mistari ya tumbo na
mwanzo wa utumbo mdogo na hivyo kuchangia kukuza idadi ya vidonda ndani ya
tumbo na hivyo kuzidisha maumivu. H. pylori husambazwa kwa njia ya maji taka na
machafu, chakula kisichopikwa vyema, au vifaa vichafu vya kulia.
Ongeza
kinga ya mwili kwa kuachana na mwenendo mbovu wa maisha yako nikimaanisha namna
ya kuishi wewe kama wewe. Pia kuachana na tabia mbaya kama uvutaji wa sigara (smoking), ulevi na kuwa katika sehemu
zenye kemikali zinazoharibu mwili (toxic
exposure). Usitumie vyakula vya kutengenezwa (processed food), sio vizuri.
Hivyo
kama unavyo vidonda vya tumbo ni vyema ukaenda hospitali kupata matibabu kama
tayari ulishajihusisha na tabia tajwa hapo juu. Usiwe mwoga wa sindano. Jikaze, nenda
hospitali.
4.
Kula
lishe bora na achana na Processed foods.
Ushazoea
chipsi, mahanjumati ya kununuliwa supermarket, basi utafiti unasema ni afadhali
kula chipsi zilizotengenezwa ukiona pale mjini – ingawa haishauriwi kuliko kula
vyakula vya kutengeneza kama nyama, nyanya, matunda kama apples, mboga za majani kama kabichi za kutengeneza n.k huongeza
vidonda vya tumbo kwa kuwa havimengenywi ipaswavyo na hukosa virutubisho vyote
muhimu.
Ukiachana
na hilo, kuna lile tulilozoea wengi wetu kwamba kuna kuruka mlo mmoja wa siku
hasa ule wa mchana. Basi tambua kwamba kula chakula mara mbili – asubuhi na
jioni – kwa siku na kuruka mlo mmoja hasa wa mchana huongeza kwa kasi kubwa
idadi ya vidonda ndani ya tumbo kwa hiyo usijidanganye kula chakula kilicho
shiba asubuhi na jioni ndio kwamba unazuia kupata vidonda vya tumbo.
Kulingana na Jackson
Seigelbaum Gastroenterology Center, vyakula ambavyo hutoa hali nzuri ya
tumbo kufanya kazi kawaida huhusisha;
i.
Vinywaji vyenye Caffeine
ii.
Pilipili manga (red/hot pepper) na chili
powder
iii. Kahawa kali (decaffeinated coffee/tea)
iv. Pombe na vilevi
v.
Cocoa, chocolate na vinywaji vyenye cola
vi. Limau, ndimu n.k na juisi zake (citrus fruits)
vii. Black
pepper
Jitahidi
kuepukana na vyakula vya namna hii na jihusishe zaidi na lishe iliiyobora yenye
mboga mboga zisizo za kutengeneza, nyama kutoka buchani sio dukani, na chakula
kilichopikwa vyema kabisa au kula lishe ya mediterani (Mediterranean
diet).
Kama ulcers
zako husababisha kutapika na kichefuchefu, ni vyema sana ukaepusha kupungukiwa
na maji mwilini (dehydration), electrolyte imbalances na upungufu wa
madini hitajika mwilini (nutrient
deficiencies).
USHAURI MWINGINE JUU YA KUENDESHA LISHE YAKO;
USHAURI MWINGINE JUU YA KUENDESHA LISHE YAKO;
i. Jitahidi kuwa na uzito
utakaoshauriwa na daktari na zuia unene wa kupindukia (obesity).
ii.
Epusha unywaji wa pombe na
uvutaji wa sigara
iii. Epusha
vya moto sana
iv. Kula
vyakula vidogo vidogo katikati ya siku
Hivyo ndivyo
utakavyoweza kupunguza kuwa na maumivu makali ya sehemu usiyoweza kuishika na
wala hushauriwi kujaribu kupachokoza hapo kwa kuwa ni kati ya sehemu nyeti sana
za mwili wako ambazo huweza kukusababishia kifo mara tu utakapopatibua.
Tuambie, unafikiri nini juu ya mada hii!
Tuambie, unafikiri nini juu ya mada hii!
Comments