JINSI YA KUFAULU MASOMO YA SCIENCE NA MATHEMATICS

JINSI YA KUFAULU MASOMO YA SCIENCE NA MATHEMATICS.

Mwanafunzi hana budi kutambua kwamba wanadamu tunaelekea ulimwengu wa aina gani. Sayansi ni kati ya sehemu inayojenga ulimwengu huo na kwetu sisi Watanzania, hatuna budi kuipenda sayansi inayokuwa kwa kasi.

Ugunduzi wa mambo mbalimbali ndiyo unaohitajika kwa sasa ili kuifanya nchi yetu ifikie nafasi tunayoitafuta 2nd World Country.


Wanafunzi tulio wengi husema kwamba Sayansi ni ngumu kuliko Arts na Biashara lakini ndani ya mioyo yetu tunatambua kwamba sio kweli. 

Kama huamini muuluze mwanafunzi mwenzako kati ya kuweka matukio yaliyopita yaliyofanyika hapo zamani kichwani mwakona kufanya hesabu juu ya Moles za Liquid H na kupiga Hesabu ya Jinsi ya kupata umbali kutoka Point A kwenda Point B Kati ya sababu zinazopelekea tukajiwekea fikra za namna hiyo ni kwamba;

 01. Si rahisi kuonekana.
Nikimaanisha kwamba si rahisi kwa sisi kuyaona yanayozungumziwa na yanayosemwa. Kwa kawaida huitwa Kusadikika kwa sababu ni THEORY. Hatuna budi tukiwa na lengo la kufauli masomo haya, Kuyaangalia kwa jicho la tatu.

02. Ni vigumu kuelezea.
Ni ngumu kuiweka wazi hasa kwa walimu wasio wazoefu na masomo yenyewe. Simaanishi hawajui, bali hawana uwezo wakuorodhesha wanayofundisha kwa wanafunzi, hivyo ni vigumu kwa wanafunzi kusema tumeelewa kutoka moyoni. Mwalimu anahitaji kulijua somo analofundisha kutoka moyoni ili aweze kuwaimarishia wanafunzi msingi wa kuyapenda masomo hayo.

03. Upeo wa CALCULATIONS!
Calculate(Kokotoa)!!! Ni neno rahisi sana lakini ni zito kuliweka kwa vitendo. Hii ni kwa sababu ni kuhesabu. Kucheza na namba, ndiyo maana kuu ya neon hilo, "Finding X and Y" ndiyo mada kuu ya masomo haya na ndiyo maana watu wanashindwa kujiweka wazi kukubali kuwatafuta watu hawa wawili. Ukiweza kucheza na namba, utaweza kucheza na masomo haya yote lakini si rahisi kihivyo.

Hivyo basi, Tufanye nini?

Hizi ni mbinu chache ambazo mimi mwenyewe na kwa usaidizi kutoka kwa wakali wenzangu wa masomo haya wanazozitumia kufaulu masomo haya:

01. Kukumbuka rules, laws, na equations kwa kuelewa umuhimu wake.

Kukumbuka ni kitu kimoja na kuelewa ni kitu kingine lakini chenye uhusiano mtimilifu na unachokumbuka. Hivyo, kama unaweza kuelewa 
F=mg
(F-force; m-mass, g-gravity)

Formula hii ya NEWTON basi ni rahisi sana kuikumbuka tena bila matatizo. Hii inachangiwa pia na ufupi wake, lakini ukipewa TRIGONOMETRY ‘Identity 1’
                    Sin (A+B) = SinACosB +/- SinBCosA

Ninauhakika kwamba kuna wengi watakao changanyikiwa na wasijue cha kufanya. Hii ni kwa sababu watashindwa kuikumbuka kwenye mtihani na hata kama wataweza basi hawataweza kujua waanzie wapi kama hawatapewa vitatu au vinne kwenye swali hilo na kama wataichanganya na Trig ‘Identity 2'
                    Cos (A+B) = SinASinB +/- CosACosB

Tuliza akili, iangalie formula na usiiogope wala kupanic kwa sababu iko tu kwenye maandishi kisha ifananishe na vile unavyoelewa wewe kisha ijaribu, Nakuhakikishia kwamba ni wazi kabisa kwamba utapata swali kwa asilimia 70% au 85%.

02. Don't Give Up.

Kwa njia yeyote ile, hata kama hujawahi kufundishwa nina uhakika kwamba kujaribu kwako kwa swali lililo mbele yako bila kuogopa kutakupa nafasi nzuri ya kuweza kulitatua swali litakalofuata na kwa asilimia kubwa ukaweza kulipata. kwa nini umeliweza? ni kwa sababu hujakubali kushindwa na kitu kilichowekwa kwako.


QN:   What point will become zero velocity at a thrown up object?
ANS: The point that the object will be at zero velocity is when the object is at the maximum point on the air without contact before it begins to fall back.

Jaribu hili, tena ni rahisi sana,
QNs:
- Why does the sky happen to appear blue and not red?

-  Why does the Earth revolve around the Sun but does not revolve towards it?


03. Know the basics (Jua yote uliyoanza kufundishwa.)

Tukija kuangalia MATHS, tunaona kwamba FORM-III kwenye Sub-topic ya COMPOUND INTEREST, ukitaka swali liishe kiurahisi bila ya wewe kuanza kuzidisha namba moja-moja, unahitaji kutumia LOGARITHMS ambayo ni topic ipatikanayo FORM-II tena bila shida utaweza kulifanya swali hilo. Huo ni mfano mmoja tu.

Ukishindwa kuelewa topic ya MOLE CONCEPT ya FORM-III: CHEMISTRY, ni wazi kabisa hutaweza maswali kadha wa kadha ya Mtihani wa mwisho FORM-IV NECTA.

Hivy basi, jitahidi kwa kadri uwezavyo kuzielewa topic zote ambazo ulisha kwisha zipitia vidato vya nyuma ili uweze kuyaweza masomo ambayo tofauti kabisa na masomo mengine.

04. Maneno ya Wengi(What People say).

Wanafunzi wengi naamini kwamba tumekuwa tukisikia maneno ya waliopita kuwa MATHS ni ugonjwa wa taifa, wengine husema Topic ya CIRCLE, NA SPHERE ni ngumu sana na wengine husema PHYSICS inachanganya lakini si kweli. Kwani walio weza kufundisha Maengineer wa nchi hii, Marubani kama William Zelothe Stephen anaye endesha AIRBUS A319 na Madaktari wao wameweza vipi?

Usisikilize yaliyokwisha kusemwa kwa sababu yatakurudisha nyuma katika maendeleo yako. Shule niliyopo mimi wanafunzi waliopita FORM-IV walikuwa wakisema ACCOUNTS ni topic ngumu sana lakini nilikuja kugundua na class-mates wenzangu kwamba wale walikuwa wakipata maneno kutoka nje kwamba topic hiyo ilikuwa ngumu, na mpaka sasa, topic hiyo ndiyo inayotupa marks za kutosha.

Usisikilize watu wanaovunja moyo na sana pendelea kukaa na watu unao dhani kwamba kabisa watakusaidia kufaulu. 

05. Take your Time (Muda na Utayari).

Imesadikika kuwa ni rahisi sana kwetu sisi wanafunzi kuweza kuandika Kinjekitile Ngwale kama jibu kwenye mtihani wa History kwa kuwa hutumia muda mfupi kufikiria kuliko kujibu swali linalohitaji kucheza na namba vidoleni. 

Kwa mfano, Albert Einstein aliweza kuhakikisha kwamba Brownian motion ni kweli kwa kuweka chembechembe ndogo kwenye maji na kutengeneza Zigzag motion.

Ilichukua mda takriban miaka mitano hadi kutambua kwamba maada ilikuwa katika mfumo mtembezi endelevu hata kama ni ukuta au mbao. Kulingana na Robert Brown alihakikisha kwamba kitu chochote che maada kiko katika mfumo endelevu wa vibration at regular frequency.

Kama watu hawa wawili-Albert Einstein(1879-1955) na Robert Brown(1773-1858)- waliweza kuchukua mda kugundua na keweka wazi vitu hivi basi hata wewe waweza kutumia mifano hii katika kujiandaa kwa kusoma na kuyapenda masomo haya ili uweze kupataufaulu mzuri wa masomo haya.

06. Yapende Masomo

Kama kweli ungependa kuyafaulu haya masomo basi yapende. Najua hii itakuwa vigumu sana kukubaliana nayo hasa tukizingatia kwamba wengi wetu ni wapenzi wa ARTS (i.e Music, Movies etc).

Lakini hata kama unapenda hizi arts, basi sio kwamba huwezi kupenda na SCIENCE. Nilikuwa kati ya top 10 waliokuwa wakifeli Physics na nilikuwa mpenzi wa kuwatch movies. nilitokea kuanza kufaulu PHYSICS baada ya kuja kukutana na TV show iitwayo THE FLASH kutoka DC Int. 

Filamu hii imekuwa sababu kuu ya mimi kupenda Physics na Maths kwa sababu yenyewe inaenda sambamba na robo ya Topics nilizofundishwa tokea FORM-I hadi sasa na hata zingine kunipelekea nizijue na kunisaidia kujibu maswali ambayo kiukweli bila ya ufahamu wake nisingeyaweza. Tokea hapo niliweza kumshawishi mwalimu wangu kuweka NIKE (√) kwenye jibu langu kwa njia zangu zinazozidi hata njia alizofundisha yeye. Si kila Filamu inapotosha!

MWISHO, FINALLY.......................

Uwezo wako wewe wa kuweza kujibu mitihani ya PHYSICS, MATHEMATICS na CHEMISTRY hata BIOLOGY na GEOGRAPHY uko sasa mikononi mwako. unataka kufaulu, basi kuwatayari kufaulu ni maamuzi yako wewe mwenyewe kwa sababu hakuna atakayekutengenezea maisha yako ya baadaye bali watakusaidia tu kukuonyesha kwa kwenda na kufanya lakini sio kufanya. 

So what are you waiting for? Kick the Cs, Ds and Fs to hell and take up your rightful place to the Bs and As. That's where you belong!!!

Tafadhali weka comment juu ya jambo hili. utakuwa msaada mkubwa kwa wanafunzi wote watakao soma hapa.

Comments

NATURE said…
Good facts anf tips
NATURE said…
Good facts anf tips
Unknown said…
That is cool facts that will lead us about science subject,
Im from juhudi high school
Unknown said…
It's TRUE my fellow 255 we have to declare that
Mbonea Moses said…
Thanx to all who commented