Kama
wewe ni mpenzi wa kutazama habari zinazojiri kila siku, unaweza ukasikia leo
usiku kwenye ITV kwamba samaki
anafaa kwa afya yako, kesho katika TBC
utasikia samaki hafai katika kuishi kwako na utajiuliza mbona wanatuchanganya.
Hapana, hakuna anayekuchanganya ila tu dunia inabadilika. Cancer au Saratani ni
aina ya maradhi yanayosababishwa na kasoro ya ugawanyikaji wa seli mwilini kama
vile uvimbe au vidonda.
Uchunguzi
umefanyika kutoka vyanzo na rejeo zaidi ya 7,000
ukipewa kipaumbele na Food and
Agriculture Organization of United Nations (FAGUN) and World Health Organization (WHO) kuandaa kitabu cha kurasa 517. The Food, Nutrition, Physical
Activity and Prevention of Cancer: A Global Perspective kimeandikwa na
wanasayansi 21 chini ya World Cancer
Research Fund and The American Institute of Cancer Research.
1st
Publication ilitolewa mwaka 1997 na Dr.
Garl Harrison akiwa kama Mchunguzi wa UCLA
na member wa Institute of Medicine wakikita toleo lao la pili The
Bible of Nutrition and Cancer.
Vyanzo vingine navyo vimeonekana kuungana na
machapisho haya mawili lakini vikiongezea kuwa Wagonjwa wengi wanaopatwa na
kansa au saratani, hupatwa na tatizo hili kutokana na jinsi wanavyoishi huku
duniani.
Hakuna
hitaji la kuwa na mshangao kwa kinachojiri kila unapotazama habari usiku. Hivyo
njia zifuatazo zinaweza kukusaidia kujiepusha kupatwa na Saratani nazo nyingi huhitaji
mabadiliko ya Lifestyle yako wewe
mwenyewe.
1. Achana
na matumizi ya Tumbaku.
Kulingana na
Hospitali ya Muhimbili iliyopo Dar es Saalam, watu zaidi ya 32 wanaoenda kupewa
tiba kila mwaka huwa na ugonjwa wa Saratani ya mapafu. Tumbaku ni mmea unaotoa
majani ambayo hukaushwa na hutumika kutengenezea sigara.
Sana sana, kwa sababu tumbaku hutumika katika sigara na ndicho wanachopendea wavutaji, huwasababishia aina tofauti za saratani ambazo ni Saratani katika Ini, Kinywa, Koo, Larynx (zoloto, mwanzo wa koromeo unaohusika na kutoa sauti), Pancreas, Kibofu na Figo. Cervix (mlango mwembamba wa uzazi unaoungana na uke) na Oral cavity (mdomo) husababishwa na Xhewing Tobacco.
NB:
Kwa upande wa pili, moshi kutoka kwenye magari na mashine zingine huweza kusababisha Kansa ya Mapafu.
Ukiacha kuvuta sigara
na ukajitahidi kujiweka mbali na moshi kutoka viwandani unaweza kuepusha kansa
ya sehemu za mwili zilizotajwa hapo juu. Jinsi ya kuachana na uvutaji wa sigara
na tumbaku tazama Jinsi ya Kuachana na Tabia sugu uliyonayo.
2. Kula
lishe bora ya Afya/A Healthy Balanced Diet.
Ili kupata lishe
bora(Balanced diet), ni vyema kama
ungejitahidi kuitafuta nahuwa inapatikana kiurahisi hata kama sio kwa asilimia
mia moja lakini asilimia tisini na tano inachukua hitaji kamili kuitwa lishe
iliyokamilika. Ili uwezekupata lishe bora jitahidi kufanya vifuatavyo;
i. Kula matunda ya kutosha nay a aina tofauti na
mboga za majani. Imegundulika
kwamba, ulaji wa matunda na vyakula vinavyoujenga mwili kama Maharage, nafaka na mboga za majani husaidia mwili wako kupunguza nafasi za kuangukiwa
na Kansa. Chukua nukuu kwamba unalohitaji la kwenda kuangaliwa kama una ulcers
ili ujue unahitaji kula aina gani ya maharage au vyakula gani visivyo na gesi
za kutibua ulcers.
Jitahidi kujiepusha
na unene wa kupindukia kwa kuchagua vyakula vyenye calories kubwa kama sukari iliyosafishwa(refined sugars) na vyakula vyenye mafuta kutoka kwa wanyama.
ii. Punguza
unywaji wa pombe na vilevi.
Kwa kufanya hivyo utakuwa umefanikiwa kuepusha Saratani ya Matiti, Mapafu, Figo na Ini.
Pia saratani hizi
zinaweza kutokea kutokana kiwango unachotumia cha unywaji na pia muda uliotumia
kwa kunywa(i.e. kipindi kizima tokea uanze kunywa vilevi).
iii. Jitahidi
kujiwekea mipaka ya kula nyama.
Za kutengenezwa. Kulingana na utafiti uliofanywa na International Agency for Research on Cancer, walifikia hitimisho
kwamba ulaji mkubwa wa nyama za kutengenezwa huweza kusababisha ongezeko la
nafasi ya wewe kupata kansa/saratani.
Ushauri;

Lishe
ya Mediterani (Mediterranean diet)
huwa sana katika upande wa vyakula vya kijani (Plant based foods and fruits-matunda)
nafaka kamili, jamii kunde (Legumes)
na nuts (njugu, lozi, korosho)
NB: Watu wanaokula lishe ya Mediterani (Mediterranean
diet), kwa kawaida huchagua mafuta ya afya(healthy fats) kama Olive Oil, Siagi
na Samaki badala ya Red meat. Ukitaka kujua zaidi juu ya Lishe ya Mediterrani
tazama Jinsi
ya kupata Lishe ya Mediterrani.
3. Fanya
mazoezi kupata uzito wa kiafya na zoea mazoezi.
Imejulikana kwamba
mazoezi yamewapelekea watu wengi kuwa na nguvu kubwa ya mwili kupingana na
maradhi tofauti lakini tatizo linakja kwamba wengi wetu wanadamu ni wavivu wa
mazoezi na ni kwa sababu wengi hukosa nafasi wakibanwa na kazi zinazowahitaji
kukaa ofisini masaa zaidi ya kumi na mbili(12).
Kufanya mazoezi
kunaweza basi kupunguza aina fulani za saratani kama ya Matiti, Prostate (tezi ya kiume isaidiayo kuunda manii), Mapafu,
Saratani ya Utumbo mpana na Figo.
Jitengenzee ratiba nzuri ya kukufanya
uwe na huo wakati wa kufanya mazoezi ya aina yoyote.
4. Jilinde
mbali na mwanga mkali wa jua.
Kujilinda na mwanga
mkali wa jua kunakuepusha na kupatwa na UV
(Ultra-Violet) Light Rays (Mionzi mikali ya jua) ambayo hushindikana
kuzuiwa na Ozone Layer-Ozoni) na
kutufikia sisi huku chini. Mionzi hii hupelekea kupata Saratani ya Ngozi na magonjwa ya macho kama
kutokuona vizuri kwa sababu ya mwanga mkali.
i Jiepushe mara kwa mara na jua la mchana ambalo
ndilo mara kwa mara hubeba mionzi hii kwa kuvaa nguo zinazokwepa ngozi kuguswa
na mionzi hii.
5. Jitahidi
kupata kinga mara kwa mara (get immunized)
Kujaribu kuzuia
Cancer kunasaidia pia kupata kinga dhidi ya magonjwa yanayosababishwa na virusi
kama vile;
i. Hepatitis B:
Ugonjwa huu huongeza nafasi ya kupatwa na Saratani ya Ini. Chanjo ya ugonjwa
huu zimeshauriwa kwa,
Watu wazima ambao hupendelea kufnaya ngono (Sexually active adults) ambao wanayo
nafasi kubwa kupataMagonjwa ya zinaa
Watumiaji wazoefu wa madawa ya kawaida nay a
kulevya
Wanaume wanaopenda ngono na wanawake wengi
Watu wasiofanya usafi makini wa sehemu zao za
siri(pubic areas)
Wanaofanya kazi za kuokoa watu wanahatari ya
kushikana na damu chafu au vimiminika vya mndani ya mwili.
Chanjo yake hushauriwa kwa wasichana na wavulana wa miaka 11 hadi 12. Pia ipo chanjo ya vijana(wa kiume na kike) wa miaka 26 au chini yake katika mahospitali tofauti .
6. Jiepishe
na tabia zisizofaa.
Kuna tabia
zisizoshauriwa katika jamii ili kujiepusha na maradhi tofauti yanayoweza
kumpata mtu. Kizuri zaidi ni kwamba kwa asilimia kubwa kuna njia za kujiepusha
na maradhi hayo.
- Punguza idadi ya watu unaofanya nao tendo hilo.
- Tumia kondomu
- Watu wenye UKIMWI wanayohatari ya kupata Saratani ya Utumbo mpana na Saratani ya Ini.
-HPV mara kwa mara huambatana na Cervical cancer lakini pia inaweza ikachangia kupata saratani ya Anus (sehemu ya kutolea kinyesi), koo, Uume, na saratani ya uke.
Kuchangia vitu vyenye ncha kali kama nyembe au sindano na muathirika wa madawa hupelekea kuambukizwa ugonjwa wa UKIMWI na pia Hepatitis B na C huleta saratani ya Ini. Ukitaka uachane na uvutaji wa madawa ya kulevya tafuta usaidizi wa Madaktari.
7. Jizoeshe
kwenda kupata Body check up mara kwa mara.
Hii hukusaidia wewe
kupata kujua ni magonjwa gani yamezuka ndani ya mwili wako na kukupa matumaini
ya yale magonjwa ambayo mwili wako unaenda kupona.
Ni
wazi kwamba mpaka sasa ninaouhakika kwamba kama hutakuwa mvivu kuzingatia kati
ya haya machache niliyokuwekea mbele yako, basi na wewe utakuwa shahidi
mwingine wa kuwasaidia wale watakaohitaji kuwa kama wewe usiye umwa na cancer.
Jilinde, Jitunze, Isaidie Jamii!
Comments